10. Bwana Anakuja

1. Bwana anakuja 
   twendeni kumlaki,
   Bwana Mungu wa 
   majeshi.
   Iwasheni mioyo
   tukampokee,
   huyo Mwenye utukufu.
       /:Karibu Bwana, njoo:/ 
         Shinda pamoja nasi.

2. Wewe ndiwe Mfalme, Mfalme
   wa mbinguni,
   utulishe wenye njaa.
   Wewe ndiwe mwanga,
   sisi tu vipofu,
   tufanye tuone tena. 
         /:Karibu Bwana...

3. Wewe ndiwe njia, 
   tutakufuata,
   turudi kwa Baba yetu. 
   Wewe ndiwe kweli, 
   utuangazie,
   tusije tukapotea. 
         /:Karibu Bwana... 

4. Hosana, Hosana,
   huyo mbarikiwa, 
   anakuja kwetu sisi.
   Aja kutulisha
   na kutugawia
   matunda ya ukombozi. 
        /:Karibu Bwana...

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya