Posts

2. Hosiana, Mesiya

1. Hosiana Mesiya, aingia mjini kwake. Fagieni popote, zipambeni njia zote; Tandikeni maua, aingie na shangwe. 2. Hosiana Mwokozi! Njoo, twakungojea Bwana Tumepamba mioyo, twakukaribisha kwetu. Tunakufungulia, milango ya mioyo 3. Hosiana, ee Shujaa! Utusaidie sisi. Tuwe wako kwa kweli, tukutumikie vema. Kwani hutakubali watu wasiokutii. 4. Hosiana Mfalme mkuu!  Uingie kwetu hima! Uliyebarikiwa, Uingie mlango wetu. Hosiana, karibu! Bwana, njoo! Haleluya!

3. Sayuni, ufuhi!

1. Sayuni ufurahi.   Shangilia Yerusalemu!   Yuaja Mfalme wako,   mwenye amani kwako.   Sayuni ufurahi!   Shangilia Yerusalemu. 2. Hosiana Mesiya    Utubariki sasa.    Jenga ufalme wako    Ulimwenguni mwote.    Hosiana Mesiya    Utubariki sasa. 3. Hosiana pongezi!    Twakuamkia Bwana!    Kiti cha enzi yako    chasimama milele.    Hosiana pongezi!    Twakuamkia Bwana.

4. Fungua Milango Yote

1. Fungua milango yote,   yuaja Bwana wa mbingu.   Mfalme wa wafalme wote,   Mwokozi wa ulimwengu.     Atuletea uzima;   kwa hiyo tumwimbieni:   Tumsifuni Mungu,   aliyetuumba. 2. Ni mwenye haki na shujaa,    upole mwingi amevaa;    Rehema ni taji yake,    huruma ni fimbo yake:    Atuondolea shida.    Kwa hiyo tumwimbieni:    Tumsifuni Mungu,    Mwokozi wetu mkuu. 3. Miji na nchi huchipushwa,    afikako Mfalme huyu;    nayo mioyo huchekeshwa,    anayoingia Yesu.    Ndiye jua la furaha    linalotufurahisha.    Tumsifuni Mungu    mtunza mioyo yetu. 4. Fungua milango yote!    Tengenezeni mioyo!    Makuti yawe upole,    furaha, pendo, amani.    Mwokozi atawajia,    aleta raha, uzima.    Tumsifuni Mungu,    ni mwenye rehema. 5. Njoo, Mwokozi...

5. Nikulakije Vema

1. Nikulakije vema    Bwana wangu Yesu?    Wote wanakungoja    wapewe uzima.    Nuru yako ing’aze    hata moyo wangu.    Nijue mambo mema,    yakupendezayo. 2. Wamekutandikia    maua na nguo.    Nami nakuimbia    nyimbo za furaha.    Moyo ukupendeze    kwa sifa na nyimbo    ukakutumikie    siku zangu zote. 3. Umetoka mbinguni    ukawa maskini.    Ukaacha furaha    utupe uzima.    Na tuliponyang’anywa ufalme    na raha,    ukaja Mponya wetu     kuturudishia. 4. Nalifungwa na mwovu:    Ukanifungua.    Nikawa nimetwezwa,    ukanitukuza.    Ukanifanya mkubwa,    ukanipa mali,     zisizomalizika,    kwa kutu na wezi 5. Umenijia mimi,    sababu ya nini?    Sababu ya kupenda,    ...

6. Wakristo, Iwekeni

1. Wakristo, iwekeni    mioyo tayari.    Yesu awaingie,    ni Mwokozi wenu.     Mungu amemtuma    kwa neema na rehema,     atuletee sisi    uzima na nuru. 2. Mwokozi anakuja,    mlimieni njia!     Mioyo iwe safi     acheni matendo    yanayomchukiza.    Lijazwe kila bonde,    milima ipunguzwe    mioyoni mwenu. 3. Ukiwa mnyenyekevu,    wapendwa na Mungu.    Ukiwa na kiburi,     utaangamizwa.     Ukimtumikia,    Mungu kwa mwendo    mwema    umpendezao yeye,    Yesu akupenda.   4. Uniweke tayari    niliye maskini,    Ee Yesu siku hizi     Ingia moyoni,     ukinijia sasa.     Nami nitakusifu    kwa kinywa na moyo.

7. Moyo Wangu Sikiliza

1. Moyo wangu sikiliza,    habari njema hii,    ya wokovu mkubwa.    Sikia kuimba    kwao malaika na watu:    “Yesu azaliwa.” 2. Mponya amekuja leo     kutoka mbinguni,     aokoe watu.    Mungu wetu ameshuka,    akawa mwana mtu    kwa ajili yetu. 3. Na sasa yumo zizini,    aita: “njooni,    hima kwangu wote,     Nawaondolea ninyi     uchungu wowote,     muwe na furaha.” 4. Basi tumwendee hima     wakubwa wadogo,     njooni wote sasa!    Yule anayetupenda,     tumpende na sisi,     awe mwanga wetu. 5. Wenye shida na ukiwa njooni,    awape    neema yake Mungu,     Yeye ana mali nyingi,    dhahabu na fedha     za mioyo yenu. 6. Ninakaa ulimwenguni     lakini napenda  ...