100. Mungu Tusaidie

1. Mungu tusaidie,

   sisi tunaangamia. 

   Nchi imeharibiwa

   na mwovu wake Shetani. 

   Kweli kweli ndiye Yesu 

   aliyewambwa mtini 

   penye mlima wa Golgotha 

   aokoe wenye dhambi.

 

2. Kaonyesha huruma, 

   Wayuda wakamsumbua.

   Wakampiga makofi, 

   Pilato aliamua.    

      Kweli kweli ndiye Yesu …

 

3. Yesu mwenye upendo 

   alikubali kuuawa, 

   damu ilimwagika  

   ili sisi tuokoke. 

       Kweli kweli ndiye Yesu…


4. Pale msalabani, 

   Bwana Yesu aliteswa 

   mzigo wa dhambi zetu

   ulimwangukia yeye. 

        Kweli kweli ndiye Yesu…


5. Sote na tukumbuke,

   kifo cha Mwokozi wetu.

   Alisema ya kwamba 

   jililieni wenyewe.  

        Kweli kweli ndiye Yesu…


6. Habari zilisemwa. 

   Mahali hapa hayupo, 

   ona alipokuwa, 

   jiwe limeondolewa.  

        Kweli kweli ndiye Yesu…


7. Ni ajabu kabisa

   wingu kuja kumpokea.  

   Habari ilisema 

   Yesu atarudi tena.   

        Kweli kweli ndiye Yesu…

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya