101. Moyo Wangu Amka Hima

1. Moyo wangu amka hima, 

   jua limetokea.

   Ondoka usingizini, 

   mpokee Mponya wako, 

   atokaye kaburini, 

   kashinda nguvu za kifo, watu 

   wafurahishwe.


2. Fufuka pamoja naye,

   uyaache mabaya!

   Maliza mwenendo wako 

   ukimngojea Yesu,  

   aliyekwenda mbinguni. 

   Kwa hiyo nawe ufanye 

   yampendezayo yeye.


3. Ukiwa na wasiwasi 

   Yesu anauweza: 

   Ukipatwa na huzuni,

   Yeye furaha yako. 

   Umtwike Bwana mizigo.

   Usisumbuke: yu hapa, 

   kwani amefufuka.


4. Usimwogope Shetani,  

   kifo hata kuzimu. 

   Shida za kufa nyepesi

   Mwokozi Yesu ni mzima. 

   Shujaa wetu haondoki,  

   awagombea wanyonge 

   wanaomtumaini.


Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya