102. Haleluya Tumwimbie

1. Haleluya! Tumwimbie 

   tumsifu sana Bwana wetu, 

   tumshangilie kwa shangwe. 

   Akafungwa na adui 

   alipokufa msalabani,

   lakini sasa yu hai.

   Habari njema hii: 

   Mesiya anakaa mzima kweli.

   Haleluya! Tumsifuni! 

   Tumsifuni Mungu wetu.


2. Haleluya! Tumwimbie, 

   tumsifu sana Bwana wetu, 

   tumshangilie kwa shangwe. 

   Watu wana shida sana, 

   taabu nyingi na huzuni

   mpaka watakapokufa.

   Furaha yetu hii: 

   Bwana ametoka kaburini. 

   Haleluya! Tumsifuni! 

   Tumsifuni Mungu wetu!


3. Haleluya! Tumwimbie, 

   tumsifu sana Bwana wetu, 

   tumshangilie kwa shangwe.

   Atatufufua sisi, 

   tutafika rahani kwake,

   tuishi pamoja naye. 

   Tumwamini Yeye 

   Mwokozi wetu mkuu, 

   mwenye nguvu. 

   Haleluya! Tumsifuni! 

   Tumsifuni Mungu wetu! 

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya