103. Moyo Yafurahie, yafanywayo

1. Moyo yafurahie, 

   yafanywayo leo:

   Mwanga umetokea 

   gizani mwa kufa.

   Mwokozi kalazwa, 

   tutakapozikwa, 

   roho ikiisha 

   kurudi mbinguni. 


2. Alipozikwa Yeye 

   adui acheka. 

   Lakini akashindwa: 

   Kristo afufuka. 

   Atokea shujaa 

   bendera mkononi, 

   kwani ameteka  

   mateka ya mwovu.

 

3. Ni jambo kubwa hili 

   lenye furaha kuu. 

   Sitaogopa sasa 

   uchungu wa kufa,

   na yote mengine 

   yatakayoteka 

   mali nipewayo 

   na Yesu Mwokozi.


4. Namshika siku zote 

   Mwokozi wangu mkuu. 

   Yeye ni kichwa chetu

   sisi tu viungo. 

   Dunia, makosa 

   Shetani, na kufa 

   Yeye kawashinda, 

   nami namfuata! 


5. Afika furahani 

   nami nitafika, 

   sitaona huzuni 

   na shida zozote.

   Mkubwa wangu Yesu 

   atanikingia 

   vinavyonidhuru,

   Yeye ngao yangu. 


6. Nitakapoingia 

   mbinguni, naona 

   andiko la furaha  

   linasomwa hivi: 

   Ashindaye kule 

   aingia hapa, 

   anayejidhili 

   atakuzwa hapa! 

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya