109. Tumsifu Mungu Enzini
1. Tumsifu Mungu enzini
na Mwana wake wa pekee,
aliyefanya wokovu:
Haleluya! Haleluya! Haleluya!
2. Siku ya tatu mapema,
jiwe halijaondolewa,
akafufuka mshindaji.
Haleluya! Haleluya! Haleluya!
3. Ametoka kuzimuni,
makosa hata shida zote,
zimetoweka kabisa.
Haleluya! Haleluya! Haleluya!
4. Umemwumbua Shetani,
ukamvua mapambo yake,
ukafungua kifungo.
Haleluya! Haleluya! Haleluya!
Comments
Post a Comment