11. Natoka Leo Mbinguni
1. Natoka leo mbinguni,
naleta habari njema
habari yenye furaha
kwa ninyi na watu wote.
2. Amezaliwa kitoto,
na mwanamwali Maria,
ni mtoto mzuri na mwema,
awaletea furaha.
3. Ni Yesu,
Mwana wa Mungu, Mwokozi
wa ulimwengu,
Atakayekuondoa
makosa yote na shida.
4. Awapa wote wokovu,
uliowekwa na Mungu,
mkae nanyi mbinguni
pamoja nasi milele.
5. Alama yenu iwe hii:
Zizini mtoto maskini
aliyevikwa viguo,
naye ni Bwana wa mbingu.
6. Tumsifuni sisi sote,
tuwafuate wachunga,
tuyaone yale makuu,
tuliyopewa na Mungu.
7. Yesu unipendezaye,
ugeuze moyo wangu,
uwe nyumba yako nzuri,
nisikuache daima.
8. Tumsifu Bwana wa mbingu,
aliyemtoa Mwanawe.
Tumwimbie kwa furaha,
pamoja nao malaika.
Comments
Post a Comment