110. Haleluya, Haleluya
1. Haleluya, Haleluya,
Sauti na mioyo juu,
tumwimbie Mungu nyimbo,
tumsifu na furaha,
Aliyemwaga damuye
kwa ulimwengu wote,
amefufuka kifoni
sasa Yesu Mwokozi.
2. Minyororo yake kifo
imekatika pia,
na katika wafu wote
Yee mzaliwa wa kwanza Yesu
ameshinda sasa,
nasi twashinda naye.
Ametupatia nasi
uzima wa milele.
3. Kristo afufuka kwanza
nao wengi baadaye.
Atakapokuja tena,
watatokea naye,
mavuno yatakuwako
mwisho wa ulimwengu,
watafika furahani
wote watakatifu.
4. Mwokozi amefufuka,
nasi tutafufuka.
Tunyeshee kama mvua
neema yako ee Bwana.
Tutafute yaliyo juu,
siyo ya ulimwengu,
na uzima tutapewa
naye Kristo kwa Mungu.
5. Tumsifuni, tumsifuni
Mungu wetu, apaswa.
Tumsifuni na Mwokozi,
aliyeshinda vita.
Tumsifuni naye Roho,
kisima cha mapenzi.
Tumsifuni Mungu wetu,
ni Utatu wa enzi.
Comments
Post a Comment