113. Bwana Yesu Kafufuka
1. K: Bwana Yesu kafufuka,
ametoka kaburini.
W: Haleluya, Haleluya,
ametoka kaburini
2. K: Na mashaka yalizuka,
hapakuwa tumaini,
W: Haleluya, Haleluya...
3. K: Wanawake walifika
asubuhi kaburini.
W: Haleluya, Haleluya...
4. K: Tayarini waliweka
manukato mkononi.
W: Haleluya, Haleluya...
5. K: Walitaka kuupaka
mwili mle kaburini.
W: Haleluya, Haleluya...
6. K: Nao hao walifika;
kumbe jiwe li kandoni.
W: Haleluya, Haleluya...
7. K: Kwa ukweli malaika
kasimama kaburini.
W: Haleluya, Haleluya...
8. K: Wakasema kafufuka;
enyi nyote kumbukeni.
W: Haleluya, Haleluya,
ametoka Kaburini
9. K: Wanawake wakumbuka;
wakatoka kaburini.
W: Haleluya, Haleluya...
10. K: Kweli Yesu kafufuka,
ametupa tumaini.
W: Haleluya, Haleluya...
11. K: Atazidi kwa neema
kuokoa waamini.
W: Haleluya, Haleluya...
Comments
Post a Comment