12. Njooni, Tumheshimu Yesu

1. Njooni, tumheshimu Yesu,

   tumtolee sifa zetu.

   Tumwimbie kwa furaha,

   sisi watu wa Yesu.


2. Baba amemtuma Mwana 

   atuletee uzima, 

   utakaopewa watu

   wenye shida na kufa.


3. Moyo wake watupenda

   kwa upendo amekuja,

   aokoe wenye dhambi 

   wasishindwe na mwovu.


4. Nuru imetutokea, 

   Yesu akiponda kichwa 

   cha adui wetu mkali 

   anayetudanganya.


5. Tutabarikiwa kweli,

   tukishika Neno hili,

   tukimsifu Bwana Yesu 

   kwa vinywa na mioyo.


6. Mwana mzuri Bwana Yesu, 

   twakuomba tupeleke 

   pale wakuimbiapo 

   malaika nyimbo nzuri. 

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya