122. Shujaa Mkubwa

1.  Shujaa mkubwa,

    Bwana wetu,

    leo umejikalisha 

    kitini kwa Babako. 

    Ufalme wote ni wako, 

    umeshinda maadui, hawana

    nguvu tena. Umepewa enzi

    kubwa, kufa pia na uzima,

    vyote unavitawala.


2. Malaika wote 

   wa mbingu 

   wanakusifu kwa nyimbo 

   wanakutumikia. 

   Ulipotoka mbinguni 

   ukaja kutuokoa, 

   na umerudi leo.

   Sasa, wako utukufu; 

   nasi tunakushukuru, 

   tunasifu Jina lako.


3. Twataka kutafuta tu 

   ufalme wako wa mbingu.

   Utupe nguvu zako, 

   tushike mwenendo mwema,

   tusiwe wenye kiburi 

   ila wanyenyekevu.

   Tuepuke kila kosa,

   tufuate njia yako 

   ya kuingia mbinguni.


4. Yesu mwana wa Daudi 

   uliyetupatanisha 

   na Bwana Mungu wetu. 

   Ulipokwenda mbinguni 

   umetutengenezea makao ya milele. 

   Tuongoze, tusichoke, 

   tusafiri siku zote;

   kwani watungoja kwako.


Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya