125. Tazameni, Anapaa
1. Tazameni, anapaa,
mwenye kushinda vita;
gari lake ni mawingu,
ndipo anapopita;
malaika wa mbinguni
wakimwimbia Bwana;
Amekaribishwa sasa,
kwa kufurahi sana.
2. Ni nani anayepaa,
wote wakimsifu?
Ndiye Bwana mwenye enzi,
ndiye Mungu wa Safu,
aliyeteseka kwanza
mle katika mti,
kwa kifo chake mwenyewe,
akashinda mauti.
3. Akaaga watu wake,
na akawabariki
akapaa mawinguni
na wakimwangalia,
chini hutenda ya Mungu,
yote yakatimia;
kazi yake imekwisha,
kwake amerejea.
4. Ni Kuhani wetu sasa,
yumo na damu yake,
katika patakatifu
twapatanishwa kwake;
Amefanya ukombozi
kuondoa dhambi zetu;
Mungu amemkubali
ndiye sadaka yetu.
5. Mwili ameuinua
huo wa ki-Adamu,
ndani yake sisi sote
pia tuna sehemu,
Mungu na Mtu pamoja,
yuko huko enzini
twaamini Bwana,
kwamba
tutakwenda mbinguni.
Comments
Post a Comment