127. Karibu kwangu Roho

1.  Karibu kwangu Roho 

    ingia moyoni,

    uliyeniletea uzima na raha. 

    Roho Mtakatifu wa Baba na wa Mwana 

    ufananaye nao ukaaye nao.


2. Unafundisha watu 

   kuomba vizuri, 

   wapate kusikiwa 

   na Mungu mbinguni.

   Unatuombea, hukomi, 

   mpaka Mungu atende 

   mambo yale  uliyoyaomba.


3. Wafurahisha moyo, 

   hupendi huzuni; 

   tukiwa matesoni, unatutuliza.

   Wazungumza nasi 

   kwa Neno lako tamu, 

   unatia mioyo furaha ya kweli.


4. Unatufanya sisi kuwa usharika; 

   hutaki tugombane 

   na kuchukiana.

   Wanaopigana unawapatanisha; 

   wataka wapendane 

   Wakristo wowote.


5. Ulinde nchi yetu, serikali yetu,

   tukae na amani duniani humu. 

   Uwape wakubwa, 

   pamoja na wadogo 

   uchaji na akili,

   wampendeze Mungu.


6. Katika mwendo wetu 

   utupe na sisi nguvu,

   tumshinde mwovu akitujaribu.

   Utusaidie, tushike njia yako

   na mwisho tufe vema

   tufike kwa Mungu. 


Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya