128. Roho Mtakatifu Uje
1. Roho Mtakatifu uje
utukalie na sisi,
fanya makao kwetu.
Utupe nuru ya mbingu,
ung’aze mioyo yetu,
tumtumikie Mungu.
Uje, lete utukufu
na furaha na uzima;
haya twatafuta kwako.
2. U chemchem yenye rehema,
unatunywesha hekima,
watufundisha vema,
tujue kuwaambia
wenzetu wasiojua
habari za wokovu.
Roho zetu uzifunge,
tuyatende mambo mema
wewe utukuzwe sana.
3. Umande mzuri wa mbingu,
geuza mioyo yetu,
tujae pendo lako.
Tupendane na wenzetu,
tuwafanyie mema tu
na kweli watu wote.
Kwetu uwe upendano;
kugombana kuwe mbali,
tuwe na amani daima.
4. Ututakase mioyo,
utupe nguvu rohoni,
tushike mwendo mwema.
Tusifuate kiburi,
tamaa mbaya za mwilini
na mambo ya dunia.
Roho zetu ziongozwe
zifikiri mambo yako,
mpaka tufikapo kwako.
Comments
Post a Comment