129. Twaomba Roho wa Mungu
1. Twaomba: Roho wa Mungu
Mfariji wetu mkuu,
utupe baraka.
Yesu alipotuaga,
kasema: Namtuma
Roho wangu kwenu.
2. Utuamshe wakosaji
kwa kuwa tu kondoo
waliopotea.
Uokoe ulimwengu,
umeharibika,
upate kujuta.
3. Roho wa ujuzi mwingi,
fundisha Wakristo
wampendeze Mungu.
Utufundishe kuomba
kwa Mungu vizuri,
tusikiwe naye.
4. Utusaidie sana,
tumshinde Shetani
na dunia pia.
Tusitengwe na Mwokozi,
yakija mateso, shida na huzuni
5. Twakuomba uwe nasi
tulio wanyonge tukijaribiwa.
Mwisho tutakapokufa,
tuone furaha baada ya mateso.
Comments
Post a Comment