13. Salamu, Yesu Bwanangu

1. Salamu Yesu Bwanangu, Wewe

   uzima wangu. 

   Nimekujia naleta

   vyote ulivyonipa:

   Ni moyo na mwili wangu, hata

   na mawazo yangu, 

   ndiyo heshima yangu.


2. Umezaliwa Bwanangu 

   kwa ajili ya mimi; 

   umenipenda kabisa,

   umenipa wokovu. 

   Tangu  mimi sijaumbwa, 

   umenitengenezea, 

   ukombozi wa moyo.


3. Uvuli mzito wa mauti,

   ulinifunikiza:  

   Umenitokea jua,

   waniangaza moyo. 

   Wewe Bwana umenipa nuru,

   raha na uzima. 

   Nakushukuru Bwana. 

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya