139. Mungu Atukuzwe Pekee
1. Mungu atukuzwe pekee,
shukrani zitolewe
sababu ya rehema kuu
aliyotutendea.
Mungu atupenda sana,
sababu hii ametupa
kutengemana vema.
2. Twakutukuza Baba mkuu
twakuheshimu sana,
sababu ya kutawala
zamani hata leo.
Nguvu zako haziishi
utakayo yatendeka,
Muumba wetu ndiwe.
3. Twakutukuza ee Yesu
Mwana wa Mungu wetu,
Uliyetupatanisha
na Baba mwenye enzi.
Mwana Kondoo wa Mungu,
sikia tukikuomba
Mwokozi wetu ndiwe.
4. Twakutukuza, ee Roho
uliyekuja kwetu.
Uwape nguvu Wakristo
waliokombolewa.
Utuokoe shidani.
Shetani asitushinde,
Mtuliza mioyo ndiwe
Comments
Post a Comment