15. Tawi Limechipuka

1. Tawi limechipuka

   shinani mwa Yese,

   kama tulivyopashwa 

   habari na wazee.

   Likatoa ua

   wakati wa usiku, 

   lilipochanua.


2. Isaya alitaja

   ua hilo zuri.

   Ni Yesu, Mponya wetu,

   Maria alimzaa.

   Usiku mtulivu. 

   Uwezo wake Mungu 

   umefanya hivi.

 

3. Na ua hili dogo

   lanukia vyema;  

   lang’aa kama jua 

   giza lafukuzwa.

   Ni Mwana wa Mungu 

   pia mwana Adamu; 

   Mwokozi wa watu.


4. Siku ya kufa kwetu Yesu

   tuongoze, tuiache dunia,

   twende furahani

   mbinguni kwa Mungu

   Pale tutakusifu

   Pasipo kukoma. 


Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya