16. Tunakuamkia Yesu

1. Tunakuamkia Yesu, 

   tunakupa pongezi. 

   Umezaliwa kikiwa, 

   malaika wakuabudu, 

   Uwe nasi!


2. Mwana wa Mungu 

   wa pekee, 

   Yeye ni  mgeni wetu,

   Anajiunga na sisi

   Mfalme wa kale na kale!

   Uwe nasi!


3. Ashikaye ulimwengu 

   ashikwa na Maria!

   Ni mtoto mdogo na 

   mchanga! 

   Tena ni Bwana wa 

   mbingu! Uwe nasi!


4. Nuru ya milele aja 

   kuleta mwanga wake.

   Aondoa giza lote;

   tuwe watoto wa mwanga. 

   Uwe nasi!


5. Kwetu akawa maskini 

   kwa kutuhurumia, 

   tupate mali ya mbingu,

   tuwe watoto wa Mungu.

   Uwe nasi!


6. Amefanya haya yote 

   kwa kuwa atupenda.

   Kwa hiyo furahini tu 

   na tumshukuru daima! 

   Uwe nasi! 

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya