17. Tuimbe na Kusifu

1. Tuimbe na kusifu

   kwa nyimbo za furaha:

   Yesu Bwana wetu 

   amezaliwa leo

   zizini Bethlehemu.

   Furaha ya mioyo.

   Mponya na Mwokozi,

   tunakusifu.


2. Nakutamani sana, 

   uliyetoka juu. 

   Ee Mwokozi mwema 

   tuliza moyo wangu, 

   unipe neema yako,

   Kitoto cha huruma.

   Univute juu, univute juu.


3. Rehema zake Mungu 

   ni nyingi, alimtuma 

   Mwana wake Yesu, 

   awakomboe watu, 

   atufanyie njia,

   tufike tena kwetu. 

   Kwetu ni kwa Mungu,

   kwetu kwa Mungu.


4. Na watu wakaao 

   katika giza wote 

   wanakungojea

   Wewe Mwokozi wetu, 

   na kukufurahia 

   uliyetukomboa.

   Yesu Bwana wetu twakutukuza.

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya