19. Usiku mtakatifu!

1. Usiku mtakatifu!
   Wengine walala 
   wakeshao ni Yosefu tu
   na Maria waliomlinda 
       Yesu mwana mzuri  
       Yesu mwana mzuri

2. Usiku mtakatifu!
   Wachunga wapewa 
   habari nzuri na malaika,
   zienezwe popote sasa: 
       Yesu Mponya kaja  
       Yesu Mponya kaja.

3. Usiku mtakatifu!
   Siku ya furaha 
   imetuangaza Kimungu 
   tumeupewa ukombozi 
   Kristo amefika
   Kristo amefika. 

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya