23. Msifuni Mungu, Wakristo

1. Msifuni Mungu, Wakristo,

   aliyetukuka,

   atufungulia mbingu 

      /:kumtoa mwanawe:/

 

2. Atokaye kifuani

   pa Mungu Babaye,

   alala sasa kitoto  

      /: kitupu, maskini. :/


3. Anyonya kwa mama yake,

   maziwa chakula,

   kwa kweli anatulisha 

       /:chakula cha mbingu.:/


4. Ageuza hali yake, 

   avaa mwili wetu 

   na sisi anatuvika 

       /: uzima wa Mungu. :/


5. Akawa mtumwa, na mimi

   naitwa kibwana,

   niwe nduguye na mtoto 

      /: wake Mungu Baba :/ 

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya