24. Ulimwenguni Pote
1. Ulimwenguni pote
asifiwe Mungu mkuu
amemtuma Mwokozi,
wakosaji wapone.
2. Zamani wazee wale
wameona hamu kuu,
waondoshwe makosa
na kumpata Mwokozi.
3. Abrahamu, Yakobo
na watu wa Sayuni
walimngojea sana,
sasa ametujia.
4. Karibu Mponya wangu
niondolee woga.
Ujitengenezee
njia moyoni mwangu.
5. Safisha nyumba yako
umfukuze Shetani,
yule nyoka wa kale.
Nikutumikie wee!
Comments
Post a Comment