25. Mungu ni wa Utukufu
1. Mungu ni wa utukufu
panapo mbinguni juu,
na kwao wampendezao
duniani raha kuu.
Sikieni nchi zote
huko mjini Bethlehemu:
/: Kristo amezaliwa,
Bwana wetu daima. :/
2. Watu na malaika wote
wanamtukuza Yesu,
ashukaye toka mbingu
kuwa kama maskini.
Akaacha enzi yake,
akavaa unyenyekevu:
/: Kristo amezaliwa,.. :/
3. Asifiwe Mungu Mwana
na Mwokozi wa watu,
mleta mwanga na uzima
Yesu mshinda kuzimu, Mfalme
wa utengemano
huko mjini Bethlehemu.
/:Kristo amezaliwa, ...:/
Comments
Post a Comment