33. Niende na Wachungaji

1. Niende na wachungaji 

   nimtazame Mponya wangu,

   kazaliwa duniani

   kwa kunipenda mimi.


2. Nimwimbie na malaika, 

   niusifu utukufu. 

   Anautengemaza, 

   kila moyo umpende.


3. Nikawaze na Maria 

   jambo hili la ajabu:

   Aacha mwili mzuri, 

   achukua wa kimtu.


4. Nimpelekee vipaji 

   na watambuzi wa nyota, 

   na nimpe mali yangu, 

   hata uzima nimpe.


5. Nakupenda, u Mwokozi,

   nikumbuke siku hii.

   Uje mwangu moyoni, 

   uufanye kikao. 

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya