34. Wakristo Furahini
1. Wakristo furahini,
furahini sana!
Mwaipigiwa leo
mbiu yenu njema!
Malaika wanaimba
huko juu mbinguni,
/: wanaimba vizuri
sauti ya kushangaa! :/
2. Hivi wanavyoimba:
Furahini nyote!
Acheni kuogopa,
tazameni nyote
kwani amezaliwa
Mwokozi wa pekee:
/: ni Bwana Yesu Kristo,
Mwana Mungu wetu:/
3. Shangilieni nyote
na kusikiliza.
Wapigieni nyote
mbiu na sauti kuu.
Mungu katupa sote
mtoto wa mbinguni,
/: kwa kutupenda sisi
amekuja kwetu. :/
Comments
Post a Comment