44. Mjini Mwake Daudi

1. Mjini mwake Daudi 

   bandani mwa mifugo 

   mtoto alizaliwa 

   na mamaye maskini

   Mariamu ni mama

   Yesu mwanawe mwema.


2. Yesu akawa mbinguni 

   akatoka enzini 

   hakukaribishwa chini 

   akalazwa horini 

   akaja kimaskini

   kuketi duniani.


3. Siku za ujana wake 

   akimheshimu mama  

   na kumtii katika yote 

   kama alivyosema. 

   Kila mwana na awe 

   mtii kama Yeye.


4. Amekuwa hata sasa 

   kielelezo chetu 

   alikuwa na unyonge 

   kama unyonge wetu 

   kucheka na kulia

   ni kama sisi sote.


5. Tutamwona waziwazi 

   ndiyo ahadi yake 

   sasa aketi mbinguni 

   katika enzi yake

   sote na tumwandame 

   kwani ni Mfalme wetu.


6. Tutamwona Yeye tena!

   Si katika kibanda,  

   ila juu: na sisi sote, 

   kwake tutakutana. 

   Hivyo tutakuwepo

   mbele yake daima. 

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya