46. Twendeni Tumshukuru
1. Twendeni tumshukuru
na kumwimbia Mungu,
aliyetupa roho
na nguvu mpaka leo.
2. Twaenda na kukua
miaka yetu yote.
Hivyo mwaka kwa mwaka
twafikia uzee.
3. Twaona shida nyingi,
uchungu na mateso
na vita na misiba
katika ulimwengu.
4. Kuhangaika kwetu
siku zote ni bure
asipotushikiza
Yeye atulindaye.
5. Na kama mama mwema ana
vyomlinda mtoto
katika shida zote,
asipotee njia.
6. Hivyo na Mungu wetu
hulinda watu wake,
huwakingia shida,
huzuni na misiba.
7. Leo atuingiza
katika mwaka mpya,
hachoki kutupenda,
kutufanyia mema.
8. Huruma zako ni mpya
kila panapokucha,
hizo zinakomesha
uchungu wa mioyo.
9. Utubariki sote
katika njia zetu,
wakubwa kwa wadogo
wakalishe mwangani.
10. U baba wa wakiwa,
u mshauri wa wajinga,
u Mponya wa wagonjwa,
u msaada wa maskini.
11. Na mwisho twakuomba:
Utupe Roho wako,
atufundishe hapa,
atuongoze kwako.
12. Wewe mwenye uzima
utupe haya yote
sisi Wakristo wako!
Kwani twakungojea!
Comments
Post a Comment