47. Anza Siku Yako Hii
1. Anza siku yako hii kwa Jina la Yesu;
Mwombe akujalie, usimame naye.
Kazi zako zote wee atazibariki.
Na tena ulalapo, atakuwa kwako.
2. Asubuhi mapema
umwombe Mwokozi,
akusaidie Yee shidani popote.
Atasimama kwako siku kuchwa pia,
na kumshinda Shetani akikujaribu.
3. Yesu akiwa nawe, waacha maadui,
usiogope hila zao zote mbaya.
Umtegemee Yesu,
shika mkono wake;
mtegemee Mwokozi,
Yeye atashinda.
4. Mambo yangu na shida
ninakuwekea
kama unavyopenda, zimalize zote.
Kazi yangu nianze kwa Jina la Yesu
nakuomba: njoo kwangu,
unisaidie!
Comments
Post a Comment