5. Nikulakije Vema

1. Nikulakije vema

   Bwana wangu Yesu?

   Wote wanakungoja

   wapewe uzima.

   Nuru yako ing’aze

   hata moyo wangu.

   Nijue mambo mema,

   yakupendezayo.


2. Wamekutandikia

   maua na nguo.

   Nami nakuimbia

   nyimbo za furaha.

   Moyo ukupendeze

   kwa sifa na nyimbo

   ukakutumikie

   siku zangu zote.


3. Umetoka mbinguni

   ukawa maskini.

   Ukaacha furaha

   utupe uzima.

   Na tuliponyang’anywa ufalme

   na raha,

   ukaja Mponya wetu 

   kuturudishia.


4. Nalifungwa na mwovu:

   Ukanifungua.

   Nikawa nimetwezwa,

   ukanitukuza.

   Ukanifanya mkubwa,

   ukanipa mali, 

   zisizomalizika,

   kwa kutu na wezi


5. Umenijia mimi,

   sababu ya nini?

   Sababu ya kupenda,

   uwaponye wote;

   waonao huzuni,

   kwa makosa yao,

   wakijuta kwa kweli, 

   utawapokea


6. Ushike neno hili:

   Umati wa Yesu,

   ukiwa na huzuni, 

   na shida popote.

   Usiogope kitu, 

   wokovu tayari.

   Anayetufariji,

   yu karibu sasa.

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya