50. Twapenda Ukaapo

1. Twapenda ukaapo 

   Bwana wetu enzini,

   furaha zako wewe 

   zinazipita zote.


2. Palipo pa kuomba 

   wajapo watu wako 

   na wewe Bwana upo, 

   uwakubali wote.


3. Twapenda Neno lako, 

   habari za wokovu,

   za nguvu za kushinda,

   za shangwe za mbinguni.


4. Twapenda nyimbo zako, 

   tunaziimba hapa,

   mpaka tutaziimba 

   pamoja na malaika.


5. Utujalie Yesu, 

   tuzidi kukupenda, 

   tuone uso wako 

   utakavyotakata. 

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya