51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu
1. Yesu ndiye kiongozi wangu,
kumfuata Yeye ni furaha,
ajuaye kuongoza vema,
anilinda, nisione shida,
analeta raha moyoni.
2. Bwana Yesu akiniongoza,
nitapita pori na misitu,
nitavuka mito na bahari
kwa furaha, kwani nina njia
ya kufika mjini kwa
Mungu.
3. Nikilala Yesu anilinda,
anitunza Yeye siku zote. Hata
nikifika njia panda, nikiona
shaka, aonyesha
njia ya kufikia kwake.
4. Siku zote namfuata Yeye,
sitaona kiu wala njaa;
anitunza kwa rehema nyingi:
nitaweka mikononi mwake
moyo wangu, auokoe.
Comments
Post a Comment