52. Jina Lake Yesu Tamu

1. Jina lake Yesu tamu; 

   Tukilisikia. 

   Hutupoza, tena hamu 

   hutuondolea.


2. Roho iliyoumia 

   kwalo hutibika, 

   chakula njaani pia; 

   raha, tukichoka.


3. Jina hili ni msingi,

   ngao, ngome, mwamba, 

   kwa hili napata wingi

   kwangu ni akiba.


4. Yesu, Mchunga, Rafiki,

   Mwalimu, Kuhani, 

   Mwanzo, Mwisho, Njia, Haki,

   Uzima kifoni.


5. Moyo wangu hauwezi

   kukusifu kweli, 

   Ila sifa zangu hizi,

   Bwana zikubali.


6. Na utakaponiita, 

   kuja kwako Bwana, 

   huko kwako sitaacha 

   kukusifu sana.

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya