53. Tumshukuru, Tumsifu
1. K: Tumshukuru, tumsifu
Mungu kwani ni mwema.
W: Huruma yake ipo,
Mchana na usiku.
2. K: Tangaza Jina lake,
Mungu wetu wa kweli.
W: Huruma yake …
3. K: Kajaza maajabu,
Mbinguni duniani.
W: Huruma yake ..
4. K: Kwa uwezo wake mkuu,
ameviumba vyote.
W: Huruma yake ..
5. K: Aliongoza watu,
ugenini zamani
W: Huruma yake ..
6. K: Maskani ametupa,
hapa ulimwenguni.
W: Huruma yake ..
7. K: Anawalisha watu,
hata wanyama pia.
W: Huruma yake ..
8. K: Na tumwimbie Mungu,
kwani Yeye ni mwema.
W: Huruma yake ..
Comments
Post a Comment