54. Yesu, u Nyota Kubwa
1. Yesu, u nyota kubwa,
itokayo kwa Yakobo,
moyo wangu wapenda
kukutumikia leo.
Ukubali vipaji
niviletavyo mimi.
2. Ninaleta dhahabu,
ndio kukutegemea,
nalo ni paji lako,
ulilonipa mwenyewe;
nikushike kwa kweli hata
majaribuni.
3. Nao uvumba wangu
ni maombi yangu mimi;
midomo na mioyo
isikome kuyatoa.
Uyakubali haya
kuwa uvumba mzuri.
4. Nayo majuto yangu
ndiyo manemane yako;
kwani hunipokea,
nikikujutia kweli.
Nasema kwa furaha:
Watwaa matunzo yangu!
Comments
Post a Comment