54. Yesu, u Nyota Kubwa

1. Yesu, u nyota kubwa, 

   itokayo kwa Yakobo, 

   moyo wangu wapenda 

   kukutumikia leo. 

   Ukubali vipaji 

   niviletavyo mimi.


2. Ninaleta dhahabu, 

   ndio kukutegemea,

   nalo ni paji lako, 

   ulilonipa mwenyewe;

   nikushike kwa kweli  hata

   majaribuni.


3. Nao uvumba wangu

   ni maombi yangu mimi; 

   midomo na mioyo 

   isikome kuyatoa.

   Uyakubali haya

   kuwa uvumba mzuri.


4. Nayo majuto yangu 

   ndiyo manemane yako; 

   kwani hunipokea, 

   nikikujutia kweli. 

   Nasema kwa furaha:

   Watwaa matunzo yangu! 

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya