55. Mmoja Ndiye
1. Mmoja ndiye tumpendaye,
aliyetoa mwili wake
akikubali mateso.
Twakupa mioyo yetu
Mwokozi uliyetufia,
twapenda kuwa wako tu.
Bwana tukubali! Ututengeneze
sisi wako. Nuru yako itung’aze
tusipotee gizani.
2. Sisi hatukukuita,
ila umetuita wewe,
huruma yako ni kubwa.
Nguvu zetu hazitoshi,
kukufanyia kazi njema
usipotutia nguvu.
Shida yetu sisi ndio ulegevu,
uondoe; nia zetu zigeuzwe
tufanye kazi kwa bidii.
3. Yesu, wewe umesema:
“Watenda kazi ni wachache
kwenye mavuno ya Bwana.”
Twaomba: Tutume nasi,
tualike wageni wengi,
nyumba ya Bwana ijae.
Heri watu wale uliochagua
kuja kwako kwenye raha
na furaha, milele hata milele.
4. Uwahurumie watu
walio mbali na wokovu
wanaoshikwa na giza.
Hawajasikia bado
utume mwema wa wokovu
tunaopewa na Mungu.
Jua la uzima liche hata kwao.
Njoo Mwokozi! Tangulia!
Twafuata, Ukifungua milango.
5. Tunataka kutangaza
habari ya upendo wako,
ya moyo wako wa kweli.
Tutawaonyesha watu
msalaba wako siku zote,
mpaka washindwe mioyoni.
Kwani Neno lako
lina nguvu kubwa ya kushinda.
mzigo wako ni mwepesi.
mlango wa mbingu ni wazi.
Comments
Post a Comment