56. Mmoja ni Mfalme

1.`Mmoja ni Mfalme 

   shujaa, ni mshindaji!

   Enyi adui, kimbieni tu!

   Nawe Sayuni uone furaha

   ukapumzishe kabisa moyo:

   Uzima, utengemano, furaha

   ndizo Mwokozi atakazokupa.


2. Twende kuonja maji ya uzima 

   tunayopewa na Bwana Yesu, 

   aliyesema 

   “Njooni kwangu nyote, 

    nitapumzisha mioyo yenu.”

    Nyweni, wapenzi, katika kisima

    chenye wokovu 

    wa wenye huzuni.


3. Mfalme wa mbingu 

   ataka kuwapa 

   kilemba kizuri cha urembo, 

   awawekea vitu vya milele,

   heshima hiyo ni ya kushinda.

   Vumilieni taabu na shida: 

   Yesu mwenyewe ni tuzo la vita.


4. Nguvu, ujuzi, heshima na sifa 

   ni zake Mungu 

   na Mwana wake. 

   Nami nataka kufika mbinguni! 

   Nifunguliwe mafungo yangu! 

   Mwenye upendo atanisikia.

   Wenye uzima wanamsifu

   Mungu.


Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya