58. Jina Moja ni Kubwa sana
1. Jina moja ni kubwa sana:
Ni Jina lako Bwanangu! Nasifu
Jina hili lako,
Yesu Kristo u Mwokozi.
Li tamu kwangu Jina hili,
jina jingine silijui.
2. Naliandika Jina hili
rohoni mwangu kabisa.
Silisahau siku zote,
halifutiki moyoni.
Li tamu kwangu Jina hili, jina
jingine sitafuti.
3. Jina hili ni jua langu
lawaka ndani ya roho.
Lanipa na utengemano,
lafuta makosa yote.
Li tamu kwangu Jina hili, jina
jingine sifahamu.
baadaye kwake Mungu?
4. Jina hili ni boma langu,
upanga wangu vitani,
ni ngao yangu na silaha,
lamshinda hata Shetani.
Li tamu kwangu Jina hili, jina
jingine silitaki.
5. Jina hili lanipa nguvu, niweze
kwenda kwa haki. Ujuzi wote
umo humo
katika Jina la Yesu.
Li tamu kwangu Jina hili, jina
jingine sitamani.
6. Ee Yesu, Jina lako ndilo furaha
yangu nikifa.
Ni cheti cha kuingilia
mbinguni kwa Bwana
Mungu.
Ndipo nitalisifu sana,
jina jingine silijui.
Comments
Post a Comment