59. Kazi ni Yako Bwanangu

1. Kazi ni yako Bwanangu 

   tunayoifanya;

   hakuna anayeweza 

   kuvunja kazi hii.

   Ni kama punje ya mbegu 

   ikiwa ndani ya mchanga,

   inakufa kwa kuoza;

   na hapo yabadilika, 

   inaota, yakua na kuzaa.


2. Yesu, umeteswa kwanza,

   halafu umepaa.

   Nao wakufuatao 

   wanateswa vivyo.

   Twaomba tusaidie 

   nasi tushike njia hii,

   kwa kufa kwako na sisi 

   tunatoka kaburini. 

   Tuongoze, tufike mbinguni.


3. Bwana wewe umekufa 

   kwa ajili yetu.

   Ukaweka ufufuo  

   ulipofufuka.

   Twaomba: Tuma mitume,

   wajulishe Jina lako

   mpaka mwisho wa dunia. 

   Utukubali na sisi

   kwa kazi hii, tutume,

   twakutii!


Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya