6. Wakristo, Iwekeni

1. Wakristo, iwekeni

   mioyo tayari.

   Yesu awaingie,

   ni Mwokozi wenu. 

   Mungu amemtuma

   kwa neema na rehema, 

   atuletee sisi

   uzima na nuru.


2. Mwokozi anakuja,

   mlimieni njia! 

   Mioyo iwe safi 

   acheni matendo

   yanayomchukiza.

   Lijazwe kila bonde,

   milima ipunguzwe

   mioyoni mwenu.


3. Ukiwa mnyenyekevu,

   wapendwa na Mungu.

   Ukiwa na kiburi, 

   utaangamizwa. 

   Ukimtumikia,

   Mungu kwa mwendo

   mwema

   umpendezao yeye,

   Yesu akupenda.

 

4. Uniweke tayari

   niliye maskini,

   Ee Yesu siku hizi 

   Ingia moyoni, 

   ukinijia sasa. 

   Nami nitakusifu

   kwa kinywa na moyo.


Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya