60. Ufalme wa Mungu

1. Ufalme wa Mungu 

   uenee popote!  

   Nguvu yako iokoe  

   wakaao gizani. 

   Uondoe woga wote,

   ukawape watu uzima,

   ufalme wa Mungu.


2. Ushinde upesi!

   Uharibu ufalme

   wa Shetani duniani, 

   ndiye mfalme wa giza. 

   Nawe utamshinda yeye, 

   kwani una nguvu ya Mungu.

   Ushinde upesi!!


3. U Shujaa wa Mungu!

   Kwa rehema ya Bwana 

   urudishe watu kwako, 

   wapendane kwa moyo, 

   wawe raia wako pote.

   Ndipo utatukuzwa sana!

   U shujaa wa Mungu!


4. Duniani popote 

   Jina lako livume 

   nguvu zako zisifiwe 

   na makabila yote,

   uliowatengemaza, 

   mpaka utakapotawala 

   duniani popote!


5. Shikeni amri hii:

   Tangazeni popote 

   kwa makabila yoyote

   Neno lenye furaha,

   wapate kuokolewa. 

   Yesu alivyotuagiza. 

   Shikeni amri hii!


6. Sifuni rehema

   ya kuokoa watu! 

   Tukimtumikia Bwana, 

   azibariki kazi 

   zote za mikono yetu; 

   amani kuu iwe kwetu. 

   Sifuni rehema! 

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya