62. Uamke Kwetu Tena Roho

1. Uamke kwetu tena Roho wa 

   mashahidi wale wa kwanza,

   waliokesha siku zote, 

   waliomshinda yule adui, 

   wakihubiri Neno la Yesu 

   kwa watu wa ulimwengu wote.


2. Uwashe moto wa upendo,

   uendelee pote kuwaka. 

   Peleka watu mavunoni,

   wanaofanya kazi kwa bidii.

   Bwana mwenye mavuno, 

   tazama: 

   Watenda kazi yako ni haba.


3. Mwanao ametuagiza kuomba

   hivi kwa Jina lake, 

   na sisi wanafunzi wake,

   twashika Neno lake kwa bidii. 

   Twaomba hivi kwa moyo wote.

   Ee Bwana usikie, ufanye!


4. Utume watu wengi sana,

   walitangaze Neno kwa nguvu.

   Tusaidie, tuokoe; 

   ufalme wa Shetani uishe.

   Usimamishe, Bwana wa

   mbingu,

   ufalme wako 

   ulimwenguni!


5. Utume mwema na uende

   mahali popote huku nchini.

   Wa dini zote waingie 

   kundini mwako mwa  

   wateule. Amsha nao Wana wa ahadi na

   wa Imani zote wakutii.


Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya