65. Yesu ni Mponya

1. Yesu ni Mponya, aleta furaha! 

   Mwanzo na mwisho 

   wa vyote ndiye. 

   Mwana Adamu 

   na Mungu wa kweli

   ametujia atubariki.

   Mbingu, dunia, toeni habari: 

   Yesu ni Mponya, aleta furaha!


2. Yesu ni Mponya, aleta wokovu!

   Sikilizeni habari njema!

   Sisi tulipomwacha Mungu wetu 

   akaturudisha tena kwake. 

   Ametufanya watoto wa Mungu.

   Yesu ni Mponya, aleta wokovu.


3. Yesu ni Mponya, aleta uzima! 

   Kamba za kufa zimekatika. 

   Mwana wa Mungu  

   kumshinda Shetani, 

   awakomboe watumwa wake,

   amewapata, kawapa uhuru.

   Yesu ni Mponya, aleta uzima.


4. Yesu ni Mponya, 

   Mchungaji wa kweli, 

   anayelisha vizuri kondoo. 

   Wote walio mbali awaita, 

   awarudishe kundini mwake.

   Awakomboa kondoo kufani: 

   Yesu ni Mponya 

   Mchungaji wa kweli.


5. Yesu ni Mponya

   na Mfalme wa enzi! 

   Mbingu zimsifu na watu wamtii.

   Anageuza mioyo ya watu, hata

   na sisi tumpe yetu, 

   kwani apenda kutupa uzima.

   Yesu ni Mponya

   na Mfalme wa enzi!


6. Yesu ni Mponya

   na mwenye upendo! 

   Anatupenda kwa moyo wote. 

   Yeye mwenyewe 

   upendo wa kweli,

   aliyekufa kwa kutupenda. 

   Nasi tumpendaye 

   kwa  nguvu ya roho! 

   Yesu ni mponya na

   mwenye upendo.


Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya