66. Mfalme ni Yesu Pekee

1. Mfalme ni Yesu pekee,

   wote wanamwangukia, 

   watawalishwa na Mungu,

   Ndimi zote ziungame 

   Yesu ni Mfalme wa pekee,

   atukuzwe popote.


2. Mfalme mkubwa, watu wako 

   wakutii, wanakusifu. 

   Yesu apita wafalme,

   Yeye ndiye mkubwa sana,

   apenda kuwakomboa, 

   kwani ndiye Mwokozi.

 

3. Enyi watu mpeni mioyo,

   mnaohuzunika njooni; 

   wakiwa semeni naye, 

   kwani vyote aviweza.

   Awagawia uzima 

   wanaomngoja yeye.


4. Kama wataka uzima,

   nenda kwake, acha soni,

   Yeye anakungojea.

   Amejitoa mwenyewe, 

   wewe upate kurithi,

   mbingu ni yako sasa.


5. Nimsifuje Yesu Kristo 

   mimi vumbi, mimi jivu? 

   Nasema: Nitamtangaza 

   Kristo Yesu ndiye Bwana! 

   Na tumpende, tumheshimu 

   sifa zote zampasa.

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya