70. Twende Vitani
1. Twende vitani vitakatifu,
zikitujia, shida na taabu.
Ngurumo zivume kutia woga.
Mwiteni Mwokozi!
Yesu ni mwanga.
2. Ingawa giza lawafunika,
na raha yenu ikizimika,
na nguvu za mwovu
hazina mpaka.
Mwiteni Mwokozi …
3. Shetani aje, akijaribu
kuvunja kazi na kuharibu
hila zake zote na zitakwisha.
Mwiteni Mwokozi …
Comments
Post a Comment