72. Tumesikia Mbiu
1. Tumesikia mbiu:
Yesu, loo! Aponya;
itangazeni kote,
Yesu loo! Aponya.
Tiini amri hiyo:
nchini na baharini,
enezeni mbiu hii:
Yesu loo! Aponya.
2. Imbeni na vitani:
Yesu loo! Aponya;
kwa nguvu ya Mkombozi,
Yesu, loo! Aponya.
Imbeni wenye shida,
Unapoumwa moyo,
na kaburini imba:
Yesu, loo! Aponya.
3. Mawimbini ienee:
Yesu, loo! Aponya:
wenye dhambi jueni:
Yesu, loo! Aponya
Visiwa na viimbe,
vilindi itikeni,
nchi shangilieni:
Yesu, loo! Aponya.
4. Upepo utangaze:
Yesu, loo! Aponya;
mataifa yashangaa;
Yesu, loo! Aponya.
Milimani, bondeni,
sauti isikike
ya wimbo wa washindi:
Yesu, loo! Aponya.
Comments
Post a Comment