74. Bwana Uliyewaita Watakatifu

1. Bwana uliyewaita, 

   watakatifu wako,

   wawe mitume, wachunga,

   walishe kundi lako; 

   Wanyonge na wenye hofu

   wakawa mashujaa, 

   na wapole wa kunena

   wasiwe kunyamaa.


2. Hata leo wawataka 

   watakatifu wako, 

   nawe wauliza tena,

   ni nani aliyeko atakaye 

   nimtume afundishe vijana?

   Ni tayari, Bwana wangu, 

   Nitume mimi Bwana.


3. Nitume na mimi, Bwana, 

   kama ulivyotumwa, 

   habari ya msamaha, 

   na dhambi kutubiwa, 

   niwahubiri wakosa, 

   na waliopotea,

   wokovu u wake Bwana, 

   aliyewafilia.


4. Astahiliye hapana

   kutamka habari, 

   lakini Wewe waweza 

   kutufanya tayari

   Neno lako tulijue,

   tupe na Roho wako, 

   hayatakuwa ya bure, 

   haya maneno yako. 

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya