76. Mwana Kondoo Ayalipa

1. Mwana Kondoo ayalipa 

   madeni ya dunia. 

   Ayachukua makosa 

   ya wakosaji wote. 

   Aenda na kuugua, 

   anakubali kuchinjwa,

   furaha aziacha. 

   Wanamhukumu wampiga,

   wanamtukana wamtesa, 

   asema: Nakubali.


2. Mwana Kondoo ni Mwokozi 

   ni Mponya wa mioyo; 

   aliyetumwa na Mungu 

   awakomboe watu. 

   Mwanangu, nenda okoa 

   watoto  niliotupa. 

   Sababu ya makosa. 

   Dhambi zao ni nyingi mno;

   watolee ukombozi

   damu na mwili wako.


3. “Tayari mimi, Babangu, 

    nitwishe nichukue. 

    Maneno uyasemayo 

    nitafuata yote”.

    Pendo hili kubwa sana, 

    lamshika Baba wa mbingu 

    amtoe mwana wake.

    Pendo hili lina nguvu, 

    linamlaza kaburini 

    aletaye uzima.


4. Sitasahau pendo hili 

   Bwanangu siku zote, 

   Nitakushika daima, 

   kama unishikavyo.

   Mwanga wa roho ni wewe; 

   roho inapozimia 

   niwie moyo wangu.

   Na tuagane, Bwanangu, 

   niwe mali yako sasa

   na halafu mbinguni. 

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya