79. Nakusalimu Kichwa

1. Nakusalimu kichwa

   kilichojaa  damu, 

   kilichovikwa taji 

   la miiba mikubwa, 

   kilichopata enzi

   kwa Mungu mbinguni, 

   kitukanwacho sasa 

   matusi makali.


2. Naona uso wako 

   watemewa mate, 

   heshima yako yote 

   imeondolewa.

   Mwanga wa macho yako 

   wazimika sasa. 

   Aliyekuharibu hivi,

   ndiye nani?


3. Mateso yako Bwana,

   yanipasa mimi.

   Wewe waadhibishwa 

   kwa ajili yangu. 

   Hukumu unapata 

   iliyonipasa.

   Bwanangu nakuomba, 

   unihurumie!


4. Na mimi nasimama

   msalabani pako;

   niwe karibu kwako 

   utoapo roho; 

   ukiugua sana

   kwa teso la kufa, 

   nitakushika Bwana 

   kwa moyo wa pendo.


5. Bwana nayashukuru 

   masumbuko yako, 

   sababu ya kuteswa 

   na kufa kuchungu. 

   Wewe umenishika, 

   nami nakushika,

   kwa ajili yangu. 

   Hukumu unapata  

   iliyonipasa.

   Bwanangu nakuomba, 

   unihurumie!


6. Moyo unaposhikwa 

   na woga wa kufa, 

   usiniache Bwana 

   katika vita hii.

   Siku ya kufa kwangu

   unisaidie,

   kufa kwako kuchungu

   kutaniokoa.


7. Niwie kama ngao 

   nitakapokufa, 

   nione uso wako katika uchungu.

   Ndipo nikutazame 

   nikukumbatie! 

   Anaye kufa hivi  

   afa kwa amani. 


Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya